Wednesday, August 12, 2009

Tumepata Uzi wa mwaka,lakini.....

Naupongeza uongozi wa Simba kwa kutoa jezi za mwaka iliwashabiki wafurahi kuvaa jezi za timu yao na mapato ya timu kuongezeka. Lakini, hivi tumeshindwa kuweka nembo ya timu yetu na tangazo la wadhamini? Hivi ukikuta duka linauza jezi kama hizi bila ruhusa ya klabu utaweza kuwashtaki? na wadhamini hamuoni nao wanahitaji kuungwa mkono kwa kuweka tangazo lao ktk jezi hizi?

Saturday, August 8, 2009

Simba Day yafana, Villa yapigwa 1 - 0

Tamasha la Simba Sports Club day limefanyika leo na kufana vilivyo. Tamasha hilo lililotanguliwa burudani ya muziki, utambulisho wa wachezaji na jezi za msimu lilimaliziwa kwa mechi kati ya Sima na SC Villa ya Uganda. Katika mechi hiyo Simba iliilaza Villa kwa bao 1 - 0 lililowekwa kimiani na mchezaji mpya wa simba aliyesajiliwa kutoka SC VIlla, Hillary Echesa

Ama kweli msimu huu utakuwa moto!

Tuesday, August 4, 2009

Kwa taarifa yako!

Timu ya Simba Sports Club lipoanzishwa mwaka 1936, ilikuwa inaitwa QUEENS. Chukua hiyo shabiki wa msimbazi.

Friday, July 31, 2009

Simba sasa kama Ulaya

Uongozi wa Simba umefungua kurasa mpya ambapo kuanzia msimu huu, kutakuwa na jezi za msimu. Jezi hizo zitatambulishwa tarehe 8/8 katika siku itakayoitwa Simba Day. Siku hiyo, wachezaji wote waliosajiliwa watatambulishwa rasmi na kutakuwa na mechi ya kirafiki kati ya Simba na SC Villa ya Uganda. Vilevile Simba SC (U-20) watavaana na African Lyon (U-20).

Ikumbukwe kuwa globu hii iliwahi kuongelea suala la kuwa na jezi za msimu ili kusaidia kuinua mapato ya klabu na morali ya wachezaji wakati wa mechi. Tunaamini huu utakuwa mwanzo mzuri na miaka ijayo badala ya kuwa na Simba Day tuwe na Simba Tournament ambapo walau timu 2 bora za West / North Africa zitakuwa zikija TZ kucheza tournament na Simba pamoa na timu nyingine teule.

Thursday, July 16, 2009

Mgosi Kumfuata Henry Joseph Norway?

Musa Hassan Mgosi(pichani), mshambuliaji wa Simba na Taifa Staz, ambae ni mchezaji pekee wa Tanzania aliyechgauliwa timu ya Africa ya mashindano ya CHAN (best 16) ameitwa kwenda Norway kufanya majaribio katika timu ya Konsvinger ya huko. Ikumbukwe timu hiyo ndio imemsajili Henry Joseph wa Simba wiki 3 zilizopita. Mgosi anatazamiwa kuondoka tarehe 25 july. Kila la Kheri Mgosi.

Kocha Phiri arudi toka Zambia,mazoezi kuanza rasmi

Kocha wa Simba, Mzambia Patrick Phiri amerejea Dar es salaam leo na kukata kidomo domo cha wanaoiombea simba mabaya ambao kila siku walikuwa wakipiga kelele kuwa Phiri harudi tena. Phiri, kocha aliyewahi kuiongoza timu ya taifa ya Zambia mara 2 katika mashindano ya CAN, ametangaza kuwa mazoezo yataanza rasmi kesho hapa hapa Dar es salaam kuiandaa na ligi ya bara inayoanza tarehe 23 august.Uwanja wa ndege alipokelewa na viongozi wa simba na kundi la ushangiliaji la kidedea.

Wednesday, July 8, 2009

Hatimae Henry Joseph asaini Norway

Baada ya sintofahamu ya muda mrefu, Henry Joseph kiuongo wa Simba amesign contract ya miaka 4 na klabu ya Konsvinger ya Norway kwa dau ambalo halijawekwa wazi (undisclosed fee). Vilevile habari nlizonazo ni kuwa mchezaji mwenzie wa Simba, Mnigeria Emeh Izechukwu ataondoka muda wowote kwenda kusign mkataba kwakuwa sasa amefikisha umri a miaka 18 ambao ndio kilikuwa kikwazo.
Wazo langu nadhani ingekuwa vizuri viongozi wangeweka wazi dau walilopata wachezaji hawa kuepuka matatizo yaliyotokea wakati wa kumuuza Odhiambo kwenda APR. Mambo ya undisclosed fee huku kwetu ambako management haiko organized sidhani kama yanajenga.

Tuesday, June 30, 2009

USAJILI SIMBA HUU HAPA / HENRY KUSIGN 2 YRS NORWAY

Baada ya pilika pilika za usajili zilizojaa kila aina ya maneno, hatimae blogu ya wapenzi imefanikiwa kupata majina ya wachezaji waliosajiliwa Simba kwa ajili ya msimu 2009 / 10, ambao ni; Juma Kaseja, Danny Mrwanda (alikuwa Kuwait kwa miaka 2), Zahoro Pazi, Uhuru Seleman (Mtibwa), Amri Kiemba (Moro United), Salim Aziz (Tanga), Hillary Echesa (Kenya) na Emmanuel Okwi (Nigeria).Dany, Zahoro na Uhuru ni wachezaji wa timu ya Taifa ya Tanzania. Juhudi bado ziko mbioni kumnasa kiungo anayeng'ara kwa sasa Mwinyi Kazimoto toka JKT (Huyu ndiye aliwafunga New Zealand goli kama la Iniesta)

Habari zingine zinasema, Henry Joseph huenda akasaini mwisho wa wiki hii mkataba wa miaka 2 na timu ya Kongsvinger ya Norway (Mdau wa Norway anaweza kutusaidia hili maana labda hata magazeti ya ki Nolsk yatakuwa yameandika)

Wednesday, June 10, 2009

Uongozi Simba huu utoto sasa

Wikiendi hii uongozi wa Simba ulishindwa kumpata katibu mkuu wa kuajiriwa baada ya kutokea ugomvi katika kikao cha kamati ya utendaji kilichotakiwa kumpitisha Katibu huyo. Chanzo inasemekana ni baadhi ya wajumbe kumkataa Kaduguda, ambae inasemekana ndiye aliyeongoza katika usaili uliofanywa na kamati ya usaili. Huu mi naona ni utoto na ufinyu wa mawazo kwa viongozi wetu. Hii yote ni kutokana na kutanguliza ubinafsi badala ya maslahi ya timu. Hivi kwanini msiiamini kamati ya usaili iliyoundwa na mwenyekiti ambayo imejaa wasomi na kuongozwa na wakili aliyebobea katika sheria?kana haja gani ya kuanza kujadili tena majina yaliyopitishwa na kamati mliyoiamini wenyewe?Hamuoni mnawavunjia heshima mliowateua ktk kamati ya usaili? Kama mmeshindwa kutokana na ubinafsi wenu si bora muwape kazi hiyo recruitment agencies kama Radar, My goli au zingine wawasaidie kufanya usaili?swali linakuja,je wakichagua watu ambao sio mnalazimisha nyie washinde mtawakubali? acheni ubinafsi kuepusha simba isije ikazuiliwa kushiriki ligi kuu inayoanza Agosti.

Monday, June 8, 2009

Henry Joseph kwenda Norway Leo


Kiungo wa kutumainiwa wa Simba, Henry Joseph Shindika, anaondoka leo kwenda Norway kuanza mpira wa kulipwa katika timu ya Kongsvinger iliyoko daraja la Kwanza. Henry ataongozana na Mnigeria, Emeh Izehukwu wa Simba ambao kwa pamoja walionekana walipokwenda kufanya majaribio katika klabu ya FC Molde huko Norway ambako hawakufuzu, lakini wakaonwa na wakala wa timu ya Kongsvinger ambae aliwapeleka katika timu hiyo. Ikumbukwe timu hii ya Norway ambayo ndio inaongoza ligi kwa sasa, majuzi wali sign mkataba wa ushirikiano na timu iliyopanda ligi kuu hapa Tanzania ya African Lyon ambao watakuwa wakibadilishana ufundi, rasilimali na wachezaji. Pichani Henry akicheza mechi ya mwisho kwa timu ya Simba dhidi ya African Lyon.

Thursday, June 4, 2009

Simba kuajiri katibu mkuu Jmosi

Klabu ya Simba jumamosi hii itaweka historia kwa kuwa na katibu mkuu aliyeajiriwa kwa mara ya kwanza tangu kuanzishwa kwa timu hiyo. Uamuzi huo unafuatia maagizo ya TFF / FIFA yanayotaka timu zote zinazoshiriki ligi kuu kuwa na katibu mkuu na Mhazini mwenye ujuzi aliyeajiriwa. Waliopita mchujo na hivyo kushiriki ktk interview ya jumamosi ni Mwina Kaduguda, Michael Maurus na Hamisi Kisiwa. Wagombea hao wote wana degree angalau moja. Blogu hii ya mashabiki inawatakia kila mafanikio wagombea na yeyote atakaeshinda atumie nafasi hiyo kuendeleza Simba.

Monday, June 1, 2009

Mchezaji bora wa Taifa Cup atua Msimbazi

Salum Aziz wa Tanga, ambae ametangazwa mchezaji bora wa mashindano ya Kili Taifa Cup iliyomalizika karibuni, amejiunga na wekundu wa Msimbazi. Habari za ndani zinasema Salum amesaini mkataba wa miaka 2 huku gharama ya mkataba ikiwa ni siri. Wakati huo huo mchezaji mkongwe Ulimboka Mwakingwe ameishauri kamati ya usajili kuchanganya na wachezaji wazoefu katika usajili ili kufanya vizuri tangu mwanzo mwa msimu.

Tuesday, May 26, 2009

J.Kaseja huyoo Msimbazi tena

Blog hii imefahamishwa kwamba Juma Kaseja amesaini kuchezea Simba msimu ujao. Kaseja (pichani akisaini mkataba wa kuchezea Yanga mwaka jana) amekubali kuchezea Simba si kwa sababu ya pesa alizopewa tu, bali pia kutokana na mapenzi aliyonayo kwa timu hii. Ieleweke kuwa usajili wa mwaka huu zimeongezeka timu 2 zinazotumia pesa nyingi katika usajili, Azam (Ya Bakhresa) na African Lyon (Ya Moh'd Enterprises) ambazo zote zilikuwa zikimtaka kaseja pia. Katika hatua nyingine, Mganga wa tiba Asili (Maji Marefu) amejitolea kumlipa Kaseja 1.5M kama mshahara kila mwezi.

Thursday, May 21, 2009

Usajili

Timu ya Simba imetangaza rasmi kutumia Sh. Milioni 200 kwa ajili ya usajili wa msimu wa 2009 / 10. Usajili huo utajumuisha wachezaji 7 wapya. Kikosi kizima kitakuwa na jumla ya wachezaji 25. Kufuatana na uamuzi wa coach, timu itasajili kipa (1), Centre back (2), Midfielder (3) na mshambuliaji (1).
Katika hatua nyingine, wachezaji Henry Joseph na Emeh Izechukwu watauzwa Kwa timu ya FC Molde ya Norway mapea mwezi ujao.

Tuesday, May 19, 2009

Ukiona Kobe kainama......

Baada ya kuinama kwa miaka 3, sasa huu ni msimu wa Simba S.C, lazima tutambe Tanzania na Africa.

Jezi za Mwaka

Hivi sasa timu za Uingereza zimeanza kuonyesha jezi zao watakazotumia msimu ujao wa ligi. Mauzo ya jezi ni moja ya chanzo kizuri tu cha kipato kwa timu za Ulaya. Hivi kwani timu yetu ya Simba inashindwa nini kutengeneza jezi za mwaka mzima zitakazotumika na timu yetu halafu ziwepo na jezi za washabiki? Mbona Taifa Stars wanaweza sasa hivi?Mdhamini ambae tunaweka tangazo lake anajulikana, sasa tatizo ni nini?Mbona za Taifa stars zinanunuliwa, kwa nini tusijaribu?

Hivi karibuni ntawawekea jezi ambazo wajanja wanaziuza mjini zikiwa na nembo ya Simba S.C.

Thursday, May 14, 2009

Ni muhimu kujua

Kwamba Jengo la makao makuu ya klabu ya Simba (liko ktk archive ya blog hii) lililoko Msimbazi lilifunguliwa na Rais wa kwanza wa Zanzibar, Hayati Sheikh Abeid A. Karume tarehe 31 july 1971. Siku hii ndipo jina la Simba lilianza kutumika rasmi badala ya Sunderland kufuatia agizo la serikali kupiga marufuku utumiaji wa majina ya timu za kigeni kwa vilabu vya hapa nchini. wakati huo mwenyekiti wa Sunderland / Simba alikuwa ni marehemu Ramadhan Kirundu, ambaye pia alikuwa meya wa Dar es salaam.
?Hivi hili agizo la kutokuiga majina lilifutwa na nani?mbona siku hizi timu ziko kibao na majina hayo?

Tuesday, May 12, 2009

Kitega uchumi cha Simba

Jengo la kitega uchumi la Simba lililopo pembeni mwa makao makuu. Huu ni mmoja ya mfano wa mawazo ya ubunifu ambao viongozi wanatakiwa kuwa nayo kujiepusha na klabu kuwa omba omba. Jengo hili lilijengwa kwa mkataba na mfanyabiashara mmoja kufuatia wakati wa uongozi wa Kassim Dewji

Sunday, May 10, 2009

Pengo la Boban laonekana Taifa Stars

Pengo la Mshambuliaji wa Simba Haruna Moshi 'Boban' jana lilijidhihirisha wazi wakati Stars walipokuwa wakicheza na DRC na kufungwa 2 - 0. Stars waliotawala muda mrefu wa kipindi cha kwanza walishindwa kabisa kupenyesha mipira kwa mshambuliaji wa mwisho, kazi ambayo ilikuwa ikifanywa na Boban. Nizar Khalfan aliyecheza no.10 kuziba pengo la Boban alishindwa kabisa kuonyesha uwezo mkubwa hata akatolewa na nafasi ya yake kuchukuliwa na Musa Mgosi.

Wakati huo huo, mchezaji wa Simba Jabir Aziz alipata nafasi ya kucheza mechi yake ya kwanza kwa Taifa Stars na kuonyesha uwezo mkubwa. Jabir aliingia nafasi ya pili kuchukua nafasi ya Nurdin Bakari. Viongozi wa Simba wafanye kila juhudi kuhakikisha mchezaji huyu anabaki kuchezea Simba kwani ni hazina kubwa.

Thursday, May 7, 2009

Kikosi cha kutisha cha Simba

Hii ni timu ya Simba mwanzoni mwa miaka ya 90. Ikumbukwe 1993 chini ya Kibaden ndipo Simba iliingia fainali ya Kombe la CAF na kutoka suluhu katika mechi ya Kwanza ya Final kule Abidjan!Wa pili kulia aliyesimama ni Mohamed Mwameja, mwanzilishi wa jina la Tanzania One, alilopea kutokana na umahili wake

Wednesday, May 6, 2009

Simba, TFF wakwaruzana

Simba imeingia katika mzozo na TFF baada ya kuwakataza wachezaji wake wasishiriki mashindano ya mikoa (TAIFA cup). Viongozi wa Simba wanasema wamewapa wachezaji wao likizo ya mwezi mmoja kwa kuwa mwezi wa sita kutakuwa na mashindano ya Tusker, mwezi wa saba Kagame Cup na mwezi wa nane msimu wa ligi 2009 / 10 unaanza. Hivyo kama wachezaji watashiriki Taifa cup, ina maana hawatapumzika kwa mwaka mzima! TFF inalazimisha kuwa mchezaji ambae ataitwa na mkoa wowote akatae kwenda atapata adhabu kali!.
Nani yuko sahihi?mbona ukweli uko wazi?

Tuesday, May 5, 2009

Fununu za Usajili

Kuna fununu kuwa beki wa kutegemewa wa Taifa Stars na Yanga, Shadrack Nsajigwa yuko katika hatua za mwisho kabisa kuhamia Simba. Ikumbukwe kuwa misimu 2 iliyoisha, aliwahi kufungiwa miezi 6 na timu yake eti kwa kuwa alifungisha makusudi siku ya Simba.Alitaka kuhama mwaka jana lakini akaamua kumalizia mkataba wake uliokuwa umebakiza mwaka mmoja.

Makao makuu Msimbazi

Jengo la makao makuu ya Simba linavyoonekana kwa sasa.Kwa kweli hali yake hairidhishi ukilinganisha na hadhi ya timu, wakati umefika kwa viongozi kuonyesha ubunifu kusaka hela za kulikarabati na sio kusubiri wafadhili wajitokeze. mbona namna za kupata fedha ziko nyingi tu?Mahali lilipo ni kitega uchumi tosha kabisa.

Monday, May 4, 2009

Kikosi Cha Simba 2008 / 09

Kipa: Ally Mustapha*, Deo Mushi*, Amani Simba
Beki: Salum Kanoni, Juma Jabu, Ramadhan Chollo, Ramadhan wasso, Juma Nyoso, Kelvin Yondani*,Meshack Abel*, Deo Naftari, Victor Costa.
Viungo: Henry Joseph*, Nico Nyagawa (capt.), Jabir Aziz*, Haruna Moshi*, Ulimboka Mwakingwe, Ramadhan Chombo
Washambuliaji: Mussa Mgosi*, Moh’d Kijuso, Emeh Izechukwu (Nigerian), Orji Orbinna (Nigerian), Moses godwin

* - walioitwa karibuni katika timu ya Taifa

Sunday, May 3, 2009

Dewji akata mzizi wa fitna

Hatimae mwenyekiti wa kamati ya Usajili ya Simba, Kassim Dewji ameweka wazi kuwa hawatakuwa tayari kumsajili tena kipa JUma Kaseja, bali watawaendeleza waliopo sasa kwa kuwa wana uwezo mkubwa." Tumeamua kumwachia mwalimu Phiri achague wachezaji wote anaotaka kuwasajili na sisi tunachofanya ni kumpa mapendekezo tu. Lakini atakapoleta suala la Kaseja tutamwambia NO".
Pengine maoni ya wadau wa globu hii yamechangia kufikisha ujumbe kwa viongozi, tukaze kamba kuendelea kushauriana kwa manufaa ya timu yetu

Special kwa Mdau wa Ughaibuni

Kikosi cha Simba kilichoshika nafasi ya pili katika msimu huu 2008/09/ Mwenye suti ndiye Coach mkuu Patrick Phiri.Bahati mbaya timu zetu hazina utamaduni wa kupiga picha ya pamoja na wachezaji wote waliosajiliwa ktk msimu n kuziuza.Hii ingeweza hata kuongeza kipato kidogo.

Saturday, May 2, 2009

Basi za TBL


Mwenyekiti wa Simba akipokea mabasi toka kwa Mkurugenzi wa masoko wa TBL, D.Minja.

Friday, May 1, 2009

TBL waikabidhi Simba Sc. Mabasi 2

Mdhamini mkuu wa timu ya Simba, TBL kupitia bia yake ya Kilimanjaro leo wamewakabidhi Simba Mabasi 2 (Toyota Coaster 'mayai' na Toyota Hiace) kwa ajili ya matumizi ya shughuli za club!Kwa ujumla mabasi hayo yana thamani ya karibia Milioni 100 (kwa mujibu wa wadhamini).
Picha za mabasi hayo zitatoka soon! Watani wetu nao wamepewa mabasi kama sisi
Asante TBL

Fununu za Usajili

Kuna fununu kuwa Simba imemnasa kiungo wa kulia wa Yanga, Shamte Ally katika usajili wake. Habari hii bado ni fununu na haijathibitishwa na uongozi wala mchezaji mwenyewe.

Kaduguda amwaga cheche

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Katibu Mkuu wa klabu hiyo Mwina Kaduguda (pichani), alisema kuwa uongozi wao umejipanga kuhakikisha timu inarudisha makali yake kama ya mwaka 2003 na kufikia hatua za juu za michuano ya kombe la Shirikisho. Kaduguda, alisema kuwa Simba ndio timu pekee yenye uwezo wa kufanya vizuri kwenye michuano ya kimataifa hapa nchini, ambapo rekodi yake haijawahi kuvunjwa.


"Tumeshindwa kuiwakilisha nchi kwa zaiaid ya mwaka mmoja, kipindi tulichokuwa nje kimetufundisha mengi, nina imani tutarudi na nguvu mpya,"alisema Kaduguda

Comment: Tunawatakia viongozi wetu kila la Kheri

Simba Vs Zanzibar Heroes Kesho

Timu ya Simba kesho itajipima na timu ya taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes katika mchezo ulioandaliwa na TASWA. Ikumbukwe kuwa awali Simba ilipangwa kucheza na wachezaji wa nje ya TZ wanaocheza ligi kuu lakini wachezaji hao wanaoongozwa na wachezaji wengi wa Yanga wameingia mitini. Simba itakipiga bila wachezaji wao wote nyote walioko kambini na timu ya Taifa.
Kila la Kheri

Phiri kusaka vipaji mikoani

Kocha mkuu wa Simba, Mzambia Phiri amesema atazunguka nchi nzima kusaka wachezaji wa kukiongezea makali kikosi cha Simba.

“Nitazunguka mikoa mingi ya Tanzania ili kupata wachezaji watakaoweza kuisaidia timu yangu kucheza msimu ujao kwa ufanisi, si kwamba sina wachezaji mahiri...ukweli ni kwamba nataka kuwa na timu bora zaidi,” Alisema Phiri.

Comments: Hivi hatujafikia wakati wa kutumia Scouts kusaka wachezaji mikoani wakamletea kocha akawafanyia majaribio?Hata tukiamua kumlipa commission kidogo yule ambae mchezaji wake atasajiliwa, nadhani itasaidia sana. Halafu klabu yetu iimarishe timu ya vijana, sio kuokoteza wachezaji.tuyatumie mashindano ya Copa Cocacola kusajili timu imara ya vijana ambao tutawasajili na hata kuwauza nje kwa kuwa umri wao unaruhusu.

Thursday, April 30, 2009

Harakati za usajili zaanza!

Simba imeanza harakati za usajili wa wachezaji kwa ajili ya msimu ujao huku panga likielekea kuwapitia baadhi ya wachezaji wakiwamo Wanigeria Emeh Izichukwu na Orji Obinna.
Habari za uhakika kutoka ndani ya klabu zinasema, wengine walioko katika hatari ya kupitiwa na mchujo huo ni beki mzoefu Ramazan Wasso na kipa Amani Simba.

Simba imeamua kuwa msimu ujao inataka kusajili wachezaji wachache ambao watalipwa vizuri na kuachana na tabia ya kuwa na wachezaji wengi ambao hawatumiki na badala yake wamekuwa wakikaa benchi kwa msimu mzima.

Habari toka klabuni zinasema, wachezaji wengi wa msimu uliopita hasa wale nyota wamekuwa wakivurunda katika mechi nyingi na nia yao ni kuwapunguza na kumwachia kocha Patrick Phiri kusajili kikosi ambacho kitaleta mabadiliko.

Comments; Mi nadhani ule wakati wa viongozi / wafahili kusajili kila mtu mchezaji wake umepitwa na wakati. Kocha aamue anataka wachezaji gani, timu itafute pesa wasajiliwe.Sio ooh, huyu mchezaji wa kundi hili, huyu kaletwa na fulani...hapo hatujengi, tunabomoa timu. Halafu foreign player akisajiliwe awe na vitu tofauti na wa ndani, sio mtu kama Wasso!

Tuesday, April 28, 2009

Jamaa walipoponea tundu la sindano

Redondo akishangilia goli la kwanza alilowafunga Yanga katika mechi ya marudiano. Bahati yao refa aliwabeba kwa kuwaongezea dakika 7.

Juma Kaseja arudishwe Simba

Kama habari kuwa viongozi wa Simba wakiongozwa na Friends of Simba wana mpango wa kumrudisha tena Juma Kaseja Msimbazi. Je?Kuna umuhimu wa kutumia pesa nyingi kumsajili Juma? maana kwa sasa Ally Mustapha na Deo Dida ni makipa wazuri na wana uwezo wa kuendelea kuwa bora zaidi. Mi nadhani tungetumia pesa kusajili forward mmoja mzuri na attacking mid fielder badala ya kipa, wengine mnaonaje?

Monday, April 27, 2009

Phiri atupeleka CAF

Kama alivyoahidi alipofika, Coach Patrick Phiri ametimiza lengo lake kwa kutupeleka mashindano ya CAF kwa kupata nafasi ya pili. Ikumbukwe kuwa alikuja tukiwa tumepoteza points nyingi sana mzunguko wa kwanza. Pata habari kamili

Simba Yairarua Polisi Dodoma 2 - 0

Kwa matokeo hayo Simba sasa imekata tiketi ya kushiriki michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF), mwakani baada ya kufikisha pointi 40, huku Yanga ambayo jana pambano lao lilishindikana kufanyika kutokana na Uwanja wa Uhuru kujaa maji ikiwa mabingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom.Hadi kipindi cha kwanza kinamalizika, hakuna timu iliyoweza kuona lango la mwenzake licha ya mpira kuwa wa kasi kubwa, huku timu zote zikishambuliana kwa zamu.Kipindi cha pili kilianza kwa kasi, huku Simba ikishangiliwa na umati wa mashabiki waliokuwa wamefurika uwanjani hapo, katika dakika ya 70, alikuwa ni Haruna Moshi 'Boban' aliyeanza kuwanyanyua mashabiki wa Wekundu wa Msimbazi kwenye viti baada ya kupachika bao safi.Baada ya dakika 12 baadaye, alikuwa ni Mohammed Kijuso aliyeihakikisha Simba kushiriki michuano ya CAF mwakani baada ya kuiandikia bao la pili na la ushindi, huku Polisi Dodoma ikikata tiketi ya kushuka daraja.Mara baada ya mchezo huo kumalizika, Katibu Mkuu wa Chama cha Mkoa wa Singida (SIREFA), Hussein Mwamba, aliliambia gazeti hili kuwa, Simba itaondoka Dodoma (Jumatatu) leo, kuelekea Singida kwa ajili ya kucheza mechi moja ya kirafiki dhidi ya Timu ya Mkoa huo, Singida Shooting Stars

Karibuni

Karibuni mashabiki na wapenzi wote wa timu ya Simba Sports Club 'Mnyama' tupashane habari, kubadilishana mawazo na hata kukosoana katika blog yetu.