Thursday, June 4, 2009

Simba kuajiri katibu mkuu Jmosi

Klabu ya Simba jumamosi hii itaweka historia kwa kuwa na katibu mkuu aliyeajiriwa kwa mara ya kwanza tangu kuanzishwa kwa timu hiyo. Uamuzi huo unafuatia maagizo ya TFF / FIFA yanayotaka timu zote zinazoshiriki ligi kuu kuwa na katibu mkuu na Mhazini mwenye ujuzi aliyeajiriwa. Waliopita mchujo na hivyo kushiriki ktk interview ya jumamosi ni Mwina Kaduguda, Michael Maurus na Hamisi Kisiwa. Wagombea hao wote wana degree angalau moja. Blogu hii ya mashabiki inawatakia kila mafanikio wagombea na yeyote atakaeshinda atumie nafasi hiyo kuendeleza Simba.

No comments:

Post a Comment