Wednesday, August 12, 2009

Tumepata Uzi wa mwaka,lakini.....

Naupongeza uongozi wa Simba kwa kutoa jezi za mwaka iliwashabiki wafurahi kuvaa jezi za timu yao na mapato ya timu kuongezeka. Lakini, hivi tumeshindwa kuweka nembo ya timu yetu na tangazo la wadhamini? Hivi ukikuta duka linauza jezi kama hizi bila ruhusa ya klabu utaweza kuwashtaki? na wadhamini hamuoni nao wanahitaji kuungwa mkono kwa kuweka tangazo lao ktk jezi hizi?

Saturday, August 8, 2009

Simba Day yafana, Villa yapigwa 1 - 0

Tamasha la Simba Sports Club day limefanyika leo na kufana vilivyo. Tamasha hilo lililotanguliwa burudani ya muziki, utambulisho wa wachezaji na jezi za msimu lilimaliziwa kwa mechi kati ya Sima na SC Villa ya Uganda. Katika mechi hiyo Simba iliilaza Villa kwa bao 1 - 0 lililowekwa kimiani na mchezaji mpya wa simba aliyesajiliwa kutoka SC VIlla, Hillary Echesa

Ama kweli msimu huu utakuwa moto!

Tuesday, August 4, 2009

Kwa taarifa yako!

Timu ya Simba Sports Club lipoanzishwa mwaka 1936, ilikuwa inaitwa QUEENS. Chukua hiyo shabiki wa msimbazi.