Monday, June 1, 2009
Mchezaji bora wa Taifa Cup atua Msimbazi
Salum Aziz wa Tanga, ambae ametangazwa mchezaji bora wa mashindano ya Kili Taifa Cup iliyomalizika karibuni, amejiunga na wekundu wa Msimbazi. Habari za ndani zinasema Salum amesaini mkataba wa miaka 2 huku gharama ya mkataba ikiwa ni siri. Wakati huo huo mchezaji mkongwe Ulimboka Mwakingwe ameishauri kamati ya usajili kuchanganya na wachezaji wazoefu katika usajili ili kufanya vizuri tangu mwanzo mwa msimu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment