Friday, July 31, 2009

Simba sasa kama Ulaya

Uongozi wa Simba umefungua kurasa mpya ambapo kuanzia msimu huu, kutakuwa na jezi za msimu. Jezi hizo zitatambulishwa tarehe 8/8 katika siku itakayoitwa Simba Day. Siku hiyo, wachezaji wote waliosajiliwa watatambulishwa rasmi na kutakuwa na mechi ya kirafiki kati ya Simba na SC Villa ya Uganda. Vilevile Simba SC (U-20) watavaana na African Lyon (U-20).

Ikumbukwe kuwa globu hii iliwahi kuongelea suala la kuwa na jezi za msimu ili kusaidia kuinua mapato ya klabu na morali ya wachezaji wakati wa mechi. Tunaamini huu utakuwa mwanzo mzuri na miaka ijayo badala ya kuwa na Simba Day tuwe na Simba Tournament ambapo walau timu 2 bora za West / North Africa zitakuwa zikija TZ kucheza tournament na Simba pamoa na timu nyingine teule.

No comments:

Post a Comment