Thursday, July 16, 2009

Kocha Phiri arudi toka Zambia,mazoezi kuanza rasmi

Kocha wa Simba, Mzambia Patrick Phiri amerejea Dar es salaam leo na kukata kidomo domo cha wanaoiombea simba mabaya ambao kila siku walikuwa wakipiga kelele kuwa Phiri harudi tena. Phiri, kocha aliyewahi kuiongoza timu ya taifa ya Zambia mara 2 katika mashindano ya CAN, ametangaza kuwa mazoezo yataanza rasmi kesho hapa hapa Dar es salaam kuiandaa na ligi ya bara inayoanza tarehe 23 august.Uwanja wa ndege alipokelewa na viongozi wa simba na kundi la ushangiliaji la kidedea.

No comments:

Post a Comment