Thursday, May 14, 2009

Ni muhimu kujua

Kwamba Jengo la makao makuu ya klabu ya Simba (liko ktk archive ya blog hii) lililoko Msimbazi lilifunguliwa na Rais wa kwanza wa Zanzibar, Hayati Sheikh Abeid A. Karume tarehe 31 july 1971. Siku hii ndipo jina la Simba lilianza kutumika rasmi badala ya Sunderland kufuatia agizo la serikali kupiga marufuku utumiaji wa majina ya timu za kigeni kwa vilabu vya hapa nchini. wakati huo mwenyekiti wa Sunderland / Simba alikuwa ni marehemu Ramadhan Kirundu, ambaye pia alikuwa meya wa Dar es salaam.
?Hivi hili agizo la kutokuiga majina lilifutwa na nani?mbona siku hizi timu ziko kibao na majina hayo?

No comments:

Post a Comment