Friday, May 1, 2009

Phiri kusaka vipaji mikoani

Kocha mkuu wa Simba, Mzambia Phiri amesema atazunguka nchi nzima kusaka wachezaji wa kukiongezea makali kikosi cha Simba.

“Nitazunguka mikoa mingi ya Tanzania ili kupata wachezaji watakaoweza kuisaidia timu yangu kucheza msimu ujao kwa ufanisi, si kwamba sina wachezaji mahiri...ukweli ni kwamba nataka kuwa na timu bora zaidi,” Alisema Phiri.

Comments: Hivi hatujafikia wakati wa kutumia Scouts kusaka wachezaji mikoani wakamletea kocha akawafanyia majaribio?Hata tukiamua kumlipa commission kidogo yule ambae mchezaji wake atasajiliwa, nadhani itasaidia sana. Halafu klabu yetu iimarishe timu ya vijana, sio kuokoteza wachezaji.tuyatumie mashindano ya Copa Cocacola kusajili timu imara ya vijana ambao tutawasajili na hata kuwauza nje kwa kuwa umri wao unaruhusu.

No comments:

Post a Comment