Sunday, May 10, 2009

Pengo la Boban laonekana Taifa Stars

Pengo la Mshambuliaji wa Simba Haruna Moshi 'Boban' jana lilijidhihirisha wazi wakati Stars walipokuwa wakicheza na DRC na kufungwa 2 - 0. Stars waliotawala muda mrefu wa kipindi cha kwanza walishindwa kabisa kupenyesha mipira kwa mshambuliaji wa mwisho, kazi ambayo ilikuwa ikifanywa na Boban. Nizar Khalfan aliyecheza no.10 kuziba pengo la Boban alishindwa kabisa kuonyesha uwezo mkubwa hata akatolewa na nafasi ya yake kuchukuliwa na Musa Mgosi.

Wakati huo huo, mchezaji wa Simba Jabir Aziz alipata nafasi ya kucheza mechi yake ya kwanza kwa Taifa Stars na kuonyesha uwezo mkubwa. Jabir aliingia nafasi ya pili kuchukua nafasi ya Nurdin Bakari. Viongozi wa Simba wafanye kila juhudi kuhakikisha mchezaji huyu anabaki kuchezea Simba kwani ni hazina kubwa.

No comments:

Post a Comment