
Tuesday, May 26, 2009
J.Kaseja huyoo Msimbazi tena

Thursday, May 21, 2009
Usajili
Timu ya Simba imetangaza rasmi kutumia Sh. Milioni 200 kwa ajili ya usajili wa msimu wa 2009 / 10. Usajili huo utajumuisha wachezaji 7 wapya. Kikosi kizima kitakuwa na jumla ya wachezaji 25. Kufuatana na uamuzi wa coach, timu itasajili kipa (1), Centre back (2), Midfielder (3) na mshambuliaji (1).
Katika hatua nyingine, wachezaji Henry Joseph na Emeh Izechukwu watauzwa Kwa timu ya FC Molde ya Norway mapea mwezi ujao.
Katika hatua nyingine, wachezaji Henry Joseph na Emeh Izechukwu watauzwa Kwa timu ya FC Molde ya Norway mapea mwezi ujao.
Tuesday, May 19, 2009
Jezi za Mwaka
Hivi sasa timu za Uingereza zimeanza kuonyesha jezi zao watakazotumia msimu ujao wa ligi. Mauzo ya jezi ni moja ya chanzo kizuri tu cha kipato kwa timu za Ulaya. Hivi kwani timu yetu ya Simba inashindwa nini kutengeneza jezi za mwaka mzima zitakazotumika na timu yetu halafu ziwepo na jezi za washabiki? Mbona Taifa Stars wanaweza sasa hivi?Mdhamini ambae tunaweka tangazo lake anajulikana, sasa tatizo ni nini?Mbona za Taifa stars zinanunuliwa, kwa nini tusijaribu?
Hivi karibuni ntawawekea jezi ambazo wajanja wanaziuza mjini zikiwa na nembo ya Simba S.C.
Hivi karibuni ntawawekea jezi ambazo wajanja wanaziuza mjini zikiwa na nembo ya Simba S.C.
Thursday, May 14, 2009
Ni muhimu kujua
Kwamba Jengo la makao makuu ya klabu ya Simba (liko ktk archive ya blog hii) lililoko Msimbazi lilifunguliwa na Rais wa kwanza wa Zanzibar, Hayati Sheikh Abeid A. Karume tarehe 31 july 1971. Siku hii ndipo jina la Simba lilianza kutumika rasmi badala ya Sunderland kufuatia agizo la serikali kupiga marufuku utumiaji wa majina ya timu za kigeni kwa vilabu vya hapa nchini. wakati huo mwenyekiti wa Sunderland / Simba alikuwa ni marehemu Ramadhan Kirundu, ambaye pia alikuwa meya wa Dar es salaam.
?Hivi hili agizo la kutokuiga majina lilifutwa na nani?mbona siku hizi timu ziko kibao na majina hayo?
?Hivi hili agizo la kutokuiga majina lilifutwa na nani?mbona siku hizi timu ziko kibao na majina hayo?
Tuesday, May 12, 2009
Kitega uchumi cha Simba
Sunday, May 10, 2009
Pengo la Boban laonekana Taifa Stars
Pengo la Mshambuliaji wa Simba Haruna Moshi 'Boban' jana lilijidhihirisha wazi wakati Stars walipokuwa wakicheza na DRC na kufungwa 2 - 0. Stars waliotawala muda mrefu wa kipindi cha kwanza walishindwa kabisa kupenyesha mipira kwa mshambuliaji wa mwisho, kazi ambayo ilikuwa ikifanywa na Boban. Nizar Khalfan aliyecheza no.10 kuziba pengo la Boban alishindwa kabisa kuonyesha uwezo mkubwa hata akatolewa na nafasi ya yake kuchukuliwa na Musa Mgosi.
Wakati huo huo, mchezaji wa Simba Jabir Aziz alipata nafasi ya kucheza mechi yake ya kwanza kwa Taifa Stars na kuonyesha uwezo mkubwa. Jabir aliingia nafasi ya pili kuchukua nafasi ya Nurdin Bakari. Viongozi wa Simba wafanye kila juhudi kuhakikisha mchezaji huyu anabaki kuchezea Simba kwani ni hazina kubwa.
Wakati huo huo, mchezaji wa Simba Jabir Aziz alipata nafasi ya kucheza mechi yake ya kwanza kwa Taifa Stars na kuonyesha uwezo mkubwa. Jabir aliingia nafasi ya pili kuchukua nafasi ya Nurdin Bakari. Viongozi wa Simba wafanye kila juhudi kuhakikisha mchezaji huyu anabaki kuchezea Simba kwani ni hazina kubwa.
Thursday, May 7, 2009
Kikosi cha kutisha cha Simba

Wednesday, May 6, 2009
Simba, TFF wakwaruzana
Simba imeingia katika mzozo na TFF baada ya kuwakataza wachezaji wake wasishiriki mashindano ya mikoa (TAIFA cup). Viongozi wa Simba wanasema wamewapa wachezaji wao likizo ya mwezi mmoja kwa kuwa mwezi wa sita kutakuwa na mashindano ya Tusker, mwezi wa saba Kagame Cup na mwezi wa nane msimu wa ligi 2009 / 10 unaanza. Hivyo kama wachezaji watashiriki Taifa cup, ina maana hawatapumzika kwa mwaka mzima! TFF inalazimisha kuwa mchezaji ambae ataitwa na mkoa wowote akatae kwenda atapata adhabu kali!.
Nani yuko sahihi?mbona ukweli uko wazi?
Nani yuko sahihi?mbona ukweli uko wazi?
Tuesday, May 5, 2009
Fununu za Usajili
Kuna fununu kuwa beki wa kutegemewa wa Taifa Stars na Yanga, Shadrack Nsajigwa yuko katika hatua za mwisho kabisa kuhamia Simba. Ikumbukwe kuwa misimu 2 iliyoisha, aliwahi kufungiwa miezi 6 na timu yake eti kwa kuwa alifungisha makusudi siku ya Simba.Alitaka kuhama mwaka jana lakini akaamua kumalizia mkataba wake uliokuwa umebakiza mwaka mmoja.
Makao makuu Msimbazi

Monday, May 4, 2009
Kikosi Cha Simba 2008 / 09
Kipa: Ally Mustapha*, Deo Mushi*, Amani Simba
Beki: Salum Kanoni, Juma Jabu, Ramadhan Chollo, Ramadhan wasso, Juma Nyoso, Kelvin Yondani*,Meshack Abel*, Deo Naftari, Victor Costa.
Viungo: Henry Joseph*, Nico Nyagawa (capt.), Jabir Aziz*, Haruna Moshi*, Ulimboka Mwakingwe, Ramadhan Chombo
Washambuliaji: Mussa Mgosi*, Moh’d Kijuso, Emeh Izechukwu (Nigerian), Orji Orbinna (Nigerian), Moses godwin
* - walioitwa karibuni katika timu ya Taifa
Beki: Salum Kanoni, Juma Jabu, Ramadhan Chollo, Ramadhan wasso, Juma Nyoso, Kelvin Yondani*,Meshack Abel*, Deo Naftari, Victor Costa.
Viungo: Henry Joseph*, Nico Nyagawa (capt.), Jabir Aziz*, Haruna Moshi*, Ulimboka Mwakingwe, Ramadhan Chombo
Washambuliaji: Mussa Mgosi*, Moh’d Kijuso, Emeh Izechukwu (Nigerian), Orji Orbinna (Nigerian), Moses godwin
* - walioitwa karibuni katika timu ya Taifa
Sunday, May 3, 2009
Dewji akata mzizi wa fitna
Hatimae mwenyekiti wa kamati ya Usajili ya Simba, Kassim Dewji ameweka wazi kuwa hawatakuwa tayari kumsajili tena kipa JUma Kaseja, bali watawaendeleza waliopo sasa kwa kuwa wana uwezo mkubwa." Tumeamua kumwachia mwalimu Phiri achague wachezaji wote anaotaka kuwasajili na sisi tunachofanya ni kumpa mapendekezo tu. Lakini atakapoleta suala la Kaseja tutamwambia NO".
Pengine maoni ya wadau wa globu hii yamechangia kufikisha ujumbe kwa viongozi, tukaze kamba kuendelea kushauriana kwa manufaa ya timu yetu
Pengine maoni ya wadau wa globu hii yamechangia kufikisha ujumbe kwa viongozi, tukaze kamba kuendelea kushauriana kwa manufaa ya timu yetu
Special kwa Mdau wa Ughaibuni
Saturday, May 2, 2009
Friday, May 1, 2009
TBL waikabidhi Simba Sc. Mabasi 2
Mdhamini mkuu wa timu ya Simba, TBL kupitia bia yake ya Kilimanjaro leo wamewakabidhi Simba Mabasi 2 (Toyota Coaster 'mayai' na Toyota Hiace) kwa ajili ya matumizi ya shughuli za club!Kwa ujumla mabasi hayo yana thamani ya karibia Milioni 100 (kwa mujibu wa wadhamini).
Picha za mabasi hayo zitatoka soon! Watani wetu nao wamepewa mabasi kama sisi
Asante TBL
Picha za mabasi hayo zitatoka soon! Watani wetu nao wamepewa mabasi kama sisi
Asante TBL
Fununu za Usajili
Kuna fununu kuwa Simba imemnasa kiungo wa kulia wa Yanga, Shamte Ally katika usajili wake. Habari hii bado ni fununu na haijathibitishwa na uongozi wala mchezaji mwenyewe.
Kaduguda amwaga cheche
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Katibu Mkuu wa klabu hiyo Mwina Kaduguda (pichani), alisema kuwa uongozi wao umejipanga kuhakikisha timu inarudisha makali yake kama ya mwaka 2003 na kufikia hatua za juu za michuano ya kombe la Shirikisho. Kaduguda, alisema kuwa Simba ndio timu pekee yenye uwezo wa kufanya vizuri kwenye michuano ya kimataifa hapa nchini, ambapo rekodi yake haijawahi kuvunjwa.
"Tumeshindwa kuiwakilisha nchi kwa zaiaid ya mwaka mmoja, kipindi tulichokuwa nje kimetufundisha mengi, nina imani tutarudi na nguvu mpya,"alisema Kaduguda
Comment: Tunawatakia viongozi wetu kila la Kheri
"Tumeshindwa kuiwakilisha nchi kwa zaiaid ya mwaka mmoja, kipindi tulichokuwa nje kimetufundisha mengi, nina imani tutarudi na nguvu mpya,"alisema Kaduguda
Comment: Tunawatakia viongozi wetu kila la Kheri
Simba Vs Zanzibar Heroes Kesho
Timu ya Simba kesho itajipima na timu ya taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes katika mchezo ulioandaliwa na TASWA. Ikumbukwe kuwa awali Simba ilipangwa kucheza na wachezaji wa nje ya TZ wanaocheza ligi kuu lakini wachezaji hao wanaoongozwa na wachezaji wengi wa Yanga wameingia mitini. Simba itakipiga bila wachezaji wao wote nyote walioko kambini na timu ya Taifa.
Kila la Kheri
Kila la Kheri
Phiri kusaka vipaji mikoani
Kocha mkuu wa Simba, Mzambia Phiri amesema atazunguka nchi nzima kusaka wachezaji wa kukiongezea makali kikosi cha Simba.
“Nitazunguka mikoa mingi ya Tanzania ili kupata wachezaji watakaoweza kuisaidia timu yangu kucheza msimu ujao kwa ufanisi, si kwamba sina wachezaji mahiri...ukweli ni kwamba nataka kuwa na timu bora zaidi,” Alisema Phiri.
Comments: Hivi hatujafikia wakati wa kutumia Scouts kusaka wachezaji mikoani wakamletea kocha akawafanyia majaribio?Hata tukiamua kumlipa commission kidogo yule ambae mchezaji wake atasajiliwa, nadhani itasaidia sana. Halafu klabu yetu iimarishe timu ya vijana, sio kuokoteza wachezaji.tuyatumie mashindano ya Copa Cocacola kusajili timu imara ya vijana ambao tutawasajili na hata kuwauza nje kwa kuwa umri wao unaruhusu.
“Nitazunguka mikoa mingi ya Tanzania ili kupata wachezaji watakaoweza kuisaidia timu yangu kucheza msimu ujao kwa ufanisi, si kwamba sina wachezaji mahiri...ukweli ni kwamba nataka kuwa na timu bora zaidi,” Alisema Phiri.
Comments: Hivi hatujafikia wakati wa kutumia Scouts kusaka wachezaji mikoani wakamletea kocha akawafanyia majaribio?Hata tukiamua kumlipa commission kidogo yule ambae mchezaji wake atasajiliwa, nadhani itasaidia sana. Halafu klabu yetu iimarishe timu ya vijana, sio kuokoteza wachezaji.tuyatumie mashindano ya Copa Cocacola kusajili timu imara ya vijana ambao tutawasajili na hata kuwauza nje kwa kuwa umri wao unaruhusu.
Subscribe to:
Posts (Atom)